HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 29, 2011

KAMPENI YA "Red Alert" INAYOENDESHWA NA VODACOM TANZANIA YAKUSANYA SHILINGI 6,284,000/= MPAKA SASA....

Vodacom Tanzania inawashukuru wote ambao tayari wameshaonesha upendo wao kupitia kampeni ya “Red Alert” na kufanikisha kukusanywa shilingi 6,284,000/= kati ya December 22, hadi December 27, 2011.

Tunapenda kutoa wito wa kuendelea kuchangia Ndugu zetu waliopatwa na janga la mafuriko kwani bado wanahitaji misaada yetu,kwa Kupitia nambari ya Red Alert 15599 mteja anaweza kuchangia shilingi 500 kwa kutuma ujumbe mfupi – SMS wenye neno MAAFA na hakuna ukomo wa ujumbe na kwa njia ya m-pesa mteja anaweza kuchangia kuanzia shilingi 1,000 na zaidi kwenda nambari 155990.

Jinsi ya kuchangia kwa m-pesa

*150*00# kupata orodha ya huduma za m-pesa.

Hatua ya 2: Chagua 4 – Lipa Bili

Hatua ya 3: Weka namba ya kampuni – weka namba 155990

Hatua ya 4: Weka namba ya kumbukumbu – weka namba yako ya simu

Hatua ya 5: Weka kiasi – ni kuanzia Tsh 1,000 na kuendelea

Hatua ya 6: Weka namba yako ya siri

Hatua ya 7: Bonyeza 1 kwa kuhakikisha muamala na tayari utakuwa umeshachangia

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad