HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, July 10, 2011

demo-image

Yanga yatwaa ubingwa wa Cecafa Kagame - Castle cup 2011

_MG_9211
Wachezaji wa timu ya Yanga,wakiongozwa na Nahodha wao Shadrack Nsajigwa wakishangilia ubingwa wao walioupata jioni hii kwa kuwachabanga bao 1-0 watani wao wa jadi Simba Sc katika mashindano ya Kagame-Castle Cup 201.
_MG_9200
Waziri wa Habari,Vijana,Michezo na Utamaduni,Mh. Emmanuel Nchimbi akimkabidhi Nahodha wa Timu ya Yanga,Shadrack Nsajigwa kitita cha dola za Kimarekani elfu 30 ikiwa ni zawadi ya ushindi walioupata leo.
_MG_9132
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania,David Minja (kushoto) akimvisha medani mmoja wa wachezaji wa timu ya Al Mereikh ambao ndio walioshika nafasi ya tatu ya mashindano hayo.
_MG_9155
Wachezaji wa Simba wakipita kuchukua medali pamoja na zawadi ya ushindi wa pili.
IMG_9080
Kipa wa timu ya Simba,Juma Kaseja akiwa karuka juu kudaka mpira uliokuwa ukielekezwa langoni kwake.
IMG_8934
Mchezaji wa timu ya Simba,Kelvin Yondani (shoto) akikabana na mchezaji wa timu ya Yanga,Davies Mwape katika mchezo wa fainali za Mashindano ya Kagame-Castle cup uliomalizika jioni hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar.
IMG_8916
Mshambuliaji wa pembeni wa timu ya Yanga,Rashid Gumbo akichanja mbuga katika lango la timu ya Simba.
IMG_9045
Hivi ndivyo mambo yalivyokuwa na mpaka kupelekea ubingwa wa mashindano haya kuelekea mtaa wa Jangawani na Twiga leo.
IMG_9025
Mashabiki wa Yanga leo kwao ni sikukuu kubwa sana maana ni furaha mwanzo mwizo.
IMG_9087
Mashabiki wa Simba hali ilikuwa hivi.
IMG_9100
Kocha msaidizi wa Yanga,Fred Felix Minziro akimlalamikia muamuzi kuwa anaongeza muda mwingi sana katika dakika 30 za ziada.
IMG_8862
Mpiga picha wa Magazeti ya Tanzania Daima,Joseph Senga akilazimishwa kuondoka upande wa mashabiki wa timu ya Simba kwa madai kwamba amevalia nguo yenye rangi ya njano.jamani hivi hii kweli ni halali??
IMG_8885
Upande wa Yanga nako walianza kuwatupia makopo watu wa huduma ya kwanza wakidaiwa kuwa wamevalia nguo zenye rangi ya timu ya Simba.
IMG_8894
Hivyo nao walilazimika kuondoka uwanjani hapo kama wanavyoonekana hapa.
IMG_8951
Baadae waliombwa kurudi na ikabidi woote wakae sehemu moja ambayo ni ya upande wa Mashabiki wa Simba.
IMG_8993

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *