HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, August 29, 2010

Dr.Bilal aendeleaa kuinadi ilani ya CCM mkoani mtwara leo

Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM,Dk. Mohamed Gharib Bilal akimnadi mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtwara Vijijini, Hawa Ghasia wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika Kijiji cha Ntiniko Wilaya ya Mtwara Vijijini Mkoa wa Mtwara.
Mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal akipita katikati ya chipukizi baada ya kupokelewa katika mpaka wa Wilaya ya Mtwara Mjini na Tandahimba Mkoa wa Mtwara wakati akiwa kwenye ziara yake ya mikutano ya kampeni leo mchana.
Mgombea Mwenza wa nafasi ya urais, Dk. Mohamed Gharib Bilal akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Nanguruwe Wilaya ya Mtwara Vijijini baada ya kusimama eneo hilo wakati akielekea Kijiji cha Ntiniko katika mkutano wa kunadi Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) leo.
Wananchi wa Kijiji cha Nahyanga Wilaya ya Tandahimba Mkoa wa Mtwara, wakimsikiliza Mgombea mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal wakati wa mkutano wa kampeni.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad