2/20/2012 ~ Copyright: Othman Michuzi ~ Mtumie Rafiki Yako , Maoni: 0
Monday, February 20, 2012
MABONDIA SALEHE MKALEKWA NA ABDALAH MOHAMED (Prince Nasem) WATAMBIANA
Bondia Salehe Mkalekwa (kushoto) na Abdalah Mohamed (Prince Nasem) wakitunishiana misuri jijini Dar es salaam leo wakati wa kutambulisha mpambano wao wa ubingwa wa KG 67 Watel weight litakalofanyika feb 24.katikati ni mratibu wa mpambano huo Shabani Adiosi (Mwaya Mwaya)(Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com)
Na Mwandishi Wetu
BINGWA wa mkanda wa Shirikisho la ngumi za kulipwa Tanzania (PST) Abdalah Mohamed 'Prenc Naseem' atapanda ulingoni kutetea mkanda wake wa PST Februari 24 mwaka huu dhidi ya Salehe Mkalekwa.
Pambano hilo la ubingwa wa PST litakuwa ni pambano la uzito wa kg 57 na litashirikisha mapambano mengine manne ya utangulizi.
Akizungumza Jijini Dar es Salaam leo, Mratibu wa pambano hilo Shaban Adiosi 'Mwayamwaya' alisema pambano hilo litafanyika katika ukumbi wa New Kibeta uliopo mbagala kuu Dar es Salaam.
Alisema pambano hilo la ubingwa wa PST ni muendelezo wa shirikisho hilo kuendelea kuinua mabondia ambao hawajawa na majina makubwa ili nao waweze kufikia kiwango kizuri cha mchezo huo.
"Ubingwa huu wa PST ni maalum kwa ajili ya mabondia chipkizi na ndio maana mabondia wanaoshirikishwa wengi ni chipkizi na lengo ni kuendeleza vipaji vyao,"alisema Mwayamwaya.
Aliyataja mapambano ya utangulizi yatakayopamba pambano hilo yatakuwa kati ya Shaaban Zungu na Hasan Debe watakaopigana uzito wa kg 55,Safari Mbeyu na Ibrahim Maokola watakaopigana uzito wa kg 67, Jofrey Pacho atakayetwangana na Dickson Kawiani na Kulwa Kindondi atakayepigana na Khaji Hamisi.
Mbali na kuwepo mapambano ya ngumi kutakuwa na uuzwaji wa DVD zenye mapambano ya mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywherth,Roy Jones, Lenox Lewis,David Haye na wengine kibao ‘DVD’ hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Ngumi, Rajabu Mhamila ‘Super ‘D’.
SH. 2,000 TU KUONA MENCHI YA STARS NA DRC

Kiingilio kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya kimataifa kati ya Taifa Stars na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) itakayofanyika Februari 23 mwaka huu kitakuwa sh. 2,000 kwa viti vya kijani na bluu.
Mechi itachezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo viti hivyo vya kijani na bluu vinachukua watazamaji 36,693 ambayo ni karibu theluthi mbili ya viti vyote kwenye uwanja huo wa kisasa.
Viti vya rangi ya chungwa kiingilio ni sh. 5,000, VIP C itakuwa sh. 7,000 wakati VIP B tiketi zitauzwa kwa sh. 10,000. Kiingilio kwa viti vya VIP A kitakuwa sh. 15,000.
Kwa vile Februari 23 mwaka huu ni siku ya kazi ili kutoa fursa kwa washabiki wengi kushuhudia pambano hilo la kimataifa, mechi hiyo itaanza saa 11 kamili jioni.
Wakati Taifa Stars inayofundishwa na Jan Poulsen imeingia kambini leo na ikitarajiwa kuanza mazoezi jioni kwenye Uwanja wa Karume, DRC ambayo iko chini ya kocha Claude Le Roy inatarajia kutua nchini kesho.
Taifa Stars na DRC zinatumia mechi hiyo kunoa wachezaji wao kabla ya mechi zao za mchujo za Kombe la mataifa ya Afrika (AFCON) zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.
Katika raundi hiyo ya awali ambayo mechi zake zitachezwa Februari 29 mwaka huu, Stars itaanzia nyumbani dhidi ya Msumbiji wakati DRC inaanzia ugenini dhidi ya Seychelles.
shule za kata kukabiliwa na walimu wenye sifa
Shule za kata katika maeneo ya kaskazini magharibi mwa kanda ya kaskazini zinakabiliwa na changamoto ya walimu wenye sifa za ufundishaji hali ambayo inachangia kushuka kwa ufaulu wa wanafunzi katika shule hizo.
Mkaguzi wa shule kwa kanda ya kaskazini magharibi bw Victa Bwindiki aliyasema hayo wakati alipokuwa katika mahafali ya saba ya kidato cha sita yaliyofanyka katika shule ya arusha Modern.
Alisema kuwa shule hizo za kata mara nyingi zinapata walimu ambao hawana sifa zinazostahili hali ambayo inaibua changamoto mbali mbali katika shule hizo hivyo kufanya kurudi nyuma kitaaluma
Aliongeza kuwa walimu wa shule za kata wanatakiwa wawe na elimu ya juu sana kwa kuwa shule zote za kata zinakuwa na wanafunzi wengi hivyo ni vema wadau wa elimu wakaweka mikakati ambyo itaweza kupounguza tatizo hilo.
Vile vile alieleza kuwa mbali na tatizo hilo pia shule hizo zinakabiliwa na uhaba wa vifaa vya kufundishia haswa swala zima la vitabu kwani kitabu kimoja kinalazimika kutumiwa na wanafunzi ishirini hali ambayo inachangia kushuka kwa kiwango cha elimu.
Alisema kuwa kutokana na upungufu huo wa vitabu wanafunzi hushindwa kusoma vitabu kwa kujiamini hivyo amewaomba wazazi pamoja na wadau wote wa elimu kuhakikisha kuwa wanatoa fursa kwa shule za kata kupewa vitabu na kuhakikisha kuwa walimu wenye sifa wanapatikana.
Kwa upande wake mkuu wa shule hiyo bw Philip Wasike alisema kuwa nao wakuu wa shule wanatakiwa kujiweka utaratibu maalum wa kuwapa motisha walimu kila mara ili waweze kuongeza bidii katika ufundishaji wao.
Alisema kluwa endapo walimu watapewa motisha kila mara basi ni wazi kuwa watafundisha kwa moyo bila kujali changamoto za mazingira ambayo yanaw3akabili.
Piga Kura yako Sasa Kwa Mwanamuziki umpendaye
Piga Kura yako kwa Mwanamuzi upendaye ili aweze kushinda tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2012.ili kupiga kura yako,Bofya hiyo Link
msiba ugiriki
Jumuiya ya watanzania nchini Ugiriki inasikitika kutangaza kifo cha Mtanzania mwenzetu HAROUN ABDALLAH OTHMAN (Maarufu kwa jina la JAMHURI)kilichotokea hospitali ya Nikeas Piraeus J'mosi 18/2/2012.
Marehemu kabla ya kuwasili ugiriki alikuwa ni mkaazi wa Kikwajuni Zanzibar. Hivi sasa tupo katika harakati za michango ya kutuwezesha kumsafirisha nyumbani.
Mwenyezi Mungu amlaze mahala pema peponi Amin.
INNA LILLAH WAINNA ILAIH RAAJIUUN
Kayu Ligopora
KATIBU MKUU
Jumuiya ya watanzania Ugiriki
Rais Kikwete akabidhi kifuta machozi cha ng'ombe longido, azindua mradi wa uwezeshaji mifugo
Rais Dr.Jakaya Kikwete akiwahutubia wananchi wa Longido wakati wa hafla ya kugawa ng’ombe zaidi ya 25,000 na mbuzi zaidi ya 15,000 kwa kaya zilizoathirika kwa ukame wilayani Longido jumapili.
Mwanafunzi Godlisten Ole Olais anayesoma kidato cha pili katika shule ya Sekondari ya Longido akiteta jambo na Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete muda mfupi baada ya Rais Kikwete kuwasili katika viwanja vya sekondari hiyo kuongoza uzinduzi wa wa mradi wa serikali wa uwezeshaji mifugo(seed stock) kwa kaya za wafugaji waliopoteza mifugo yote kutokana na ukame msimu wa 2008-2009 na 2009-2010 zilizofanyika wilayani longido jumapili.
Viongozi wa kabila la Kimasai(Laigwenani) wakimpa Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete zana za kijadi za uongozi mkuki na fimbo wakati wa hafla ya kukabidhi ng’ombe iliyofanyika wilayani Longido jumapili.
Mmoja wa Wazee wa Kimasai akimuombea dua Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete wilayani Longido Jumapili.
Mzee wa Kimasai mkazi wa Longido akimshukuru na kumuombea dua njema Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete baada ya mzee huyo kukabidhiwa ng’ombe watano na mbuzi watano wilayani Longido jana.Mzee huyo ni mmoja wa wafugaji walipoteza mifugo yao yote kufuatia ukame mkali uliozikumba wilaya za Longido,Ngorongoro naMonduli.
Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi mmoja wa wakazi wa Longido ngombe watano na mbuzi katika sherehe ambayo jumla ya kaya 16 zilikabidhiwa ngombe na mbuzi baadaya kuathirika na janga la kiangazi ambapo baadhi wakazi wa wilaya za Longido,Ngorongoro na Monduli walipoteza mifugo yao yote.Katika zoezi hilo serikali imetoa jumla ya ngombe zaidi ya 25,000 na zaidi ya mbuzi 15,000 ili kuzisaidia familia hizo kuanza tena maisha yao yanayotegemea sana mifugo.Sherehe za makabidhiano hayo zimefanyika wilayani Longido, mkoani Arusha.
Morani wa kimasai wakicheza ngoma maalumu wakati wa sherehe hizo.Picha na mdau Freddy maro wa Ikulu.
Sunday, February 19, 2012
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar atembelea kijiji cha Mchekeni Kiwengwa Wilaya ya Kaskazini ‘‘B’’ kuwapa pole waliopatwa na janga la nyumba zao kuteketea kwa moto
MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI IDDI AKIMKABIDHI SHILINGI LAKI NNE {400.000/- } SHEHA WA SHEHIA YA KIWENGWA BWANA MAULIDI MASOUD AME KWA AJILI YA KUWAFARIJI WANANCHI WA MCHEKENI AMBAO NYUMBA ZAO NANE ZIMETEKETEA KWA MOTO JUMAMOSI JIONI YA TEREHE 18/2/2012.KATI KATI NI MKUU WA MKOA WA KASKAZINI UNGUJA MH. PEMBA JUMA KHAMIS.
Serikali itaangalia hali halisi ya namna gani itakavyotoa maamuzi muwafaka kuhusiana na Wananchi wanaoishi kwenye eneo lililotengwa kwa hifadhi ya Misitu liliopo Kiwengwa Pongwe.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ameeleza hayo wakati akitoa mkono wa pole kwa Familia nane za Wananchi waliokumbwa na janga la nyumba zao kuteketea kwa moto hapo Mchekeni Kiwengwa Wilaya ya Kaskazini ‘‘B’’.
Familia Tano za Wananchi hao hivi sasa zimehifadhiwa katika Jengo la Ofisi ya CCM Jimbo la Kitope iliyopo Kinduni na Tatu zilizobaki zimepata hifadhi kwa Majirani wa karibu wa Eneo hilo la Mchekeni.
Balozi Seif alisema ni vyema kwa Serikali ikatafakari kwa pamoja suala la Makaazi ya Wananchi hao sambamba na umuhimu wa hifadhi ya Misitu iliyopo katika sehemu hiyo.
“ Maamuzi yoyote yatakayotolewa na Serikali lazima myakubali. Inawezekana kuhamishwa au kuendelea kubakia hapa, lakini cha msingi zaidi ni kutolewa uwamuzi utakaolinda maslahi zaidi ya jumla ya Taifa ”. Alisisitiza Balozi Seif.
“ Hivi sasa wapo tu kama popo hawana uwezo wa kujenga makaazi ya kudumu kwa sababu eneo hilo kutangazwa kuwa Hifadhi ya Misitu ”.
Balozi Seif aliendelea kufafanua zaidi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwaeleza Wananchi hao kwamba lazima wawe na uhakika wa Maisha yao yakiambatana pia na shughukli zao za Kimaisha kama vile Kilimo na harakati za ujasiri amali.
Alisisitiza kwamba Wanakijiji hivi sasa wanashindwa na maamuzi ya ujenzi wa nyumba za kudumu kutokana na Mamlaka inayohusika na misitu kutoruhusu ujenzi katika eneo hilo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar akiwa pia ni Mbunge wa Jimbo la Kitope alitoa mchango wa Shilingi Laki Nne kuwafariji Wananchi hao kutokana na Janga hilo ili kupata kianzio cha Maisha.
Mapema Mjumbe wa Nyumba Kumi { Balozi } katika eneo hilo Nd. Elyas Yaqoub alimueleza Balozi Seif kwamba chanzo cha Moto huo ni Mtoto wa moja ya Familia zilizopata janga hilo kujaribu kusaidia harakati za mapishi kwenye nyumba yao na baadaye kushindwa kudhibiti moto aliokuwa akiuchochea jikoni hapo.
Naye Sheha wa Shehia ya Kiwengwa Bwana Maulid Masoud Ame alisema Wakaazi wa eneo hilo wanalazimika kuendelea kujenga nyumba za Makuti ambazo ni hatari kwa vile eneo hilo liko katika msongamano wa mawazo.
Bwana Maulid Alisema mbali ya suala hilo lakini hata huduma za maji zimekuwa finyu na kupelekea Wananchi hao kushindwa kukabiliana na Moto huo kutokana na ukosefu wa Maji.
Nyumba nane zilizoungua moto huo zilikuwa zikimilikiwa na Nd. Six Alfred, Kisumo Paulo, Maganga Said, Chales Lukas, Stephano Kabangara, Simon Chales, Tabia Petro na Mwashi Kabangara.
Hadi sasa hasara ya gharama ya jumla iliyotokana na kuunguwa kwa Nyumba hizo bado haijajuilikana ambapo baadhi ya Wakaazi hao wamepoteza kila kitu.
Rais Kikwete katika shamba lake la manyasi ya kulishia mifugo kijijini Msoga
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa shambani kwake Msoga, Wilaya ya Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. Shamba hilo ni la manyasi ya kulishia mifugo kwa njia ya kisasa (zero grazing), akiwa ni mmoja wa wafugaji kijijini hapo. Rais Kikwete, ambaye aghalabu hutumia muda wake wa likizo shambani kwake, pia analima pia mananasi ambayo hustawi vizuri katika wilaya hiyo.PICHA NA IKULU.
Tanzania, Comoro, Ushelisheli zasaini makubaliano ya Mpaka wa Bahari
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard Membe akishiriki utiaji saini Mkataba wa Makubaliano ya Mpaka wa Bahari wa Tanzania, Comoro na Ushelisheli. Katikati ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Ushelisheli , Jean-Paul Adam na Waziri wa Mambo ya Nje wa Comoro, Mohamed Ben Charif. Hafla hiyo ilifanyika juzi katika Ofisi ya Mambo ya Nje ya Ushelisheli mjini Mahe.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard Membe akishikana mikono na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ushelisheli, Jean-Paul Adam (kulia) na Waziri wa Mambo ya Nje wa Comoro, Mohamed Ben Charif (katikati) mara baada ya kulitiana saini Mkataba wa Makubaliano ya Mpaka wa Bahari wa Tanzania, Comoro na Ushelisheli.
Na Mwandishi Wetu
Serikali za Tanzania, Ushelisheli na Comoro zimesaini Mkataba wa Makubaliano ya Mpaka wa Bahari ya Hindi baina nchi hizo.
Utiaji saini huo ulifanyika Februari 17, mwaka huu katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Ushelisheli, mjini Mahe.
Katika hafla hiyo, Tanzania iliwakilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe; Ushelisheli iliwakilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje, Jean-Paul Adam; na Comoro ilimtuma Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano, Mohamed Ben Charif.
Baada ya kusainiwa, Hati Thibitisho hizo zitapelekwa katika Umoja wa Mataifa ambako mipaka rasmi ya nchi hizo itathibitishwa na kutambulika kimataifa.
Akizungumza katika hafla hiyo, Membe alisema kutiwa saini kwa hati hizo ni ukamilishaji kazi hiyo iliyochukua miongo miwili.
Alisema mataifa mengi ya Afrika yana migogoro ya mipaka, jambo ambalo limekuwa likisababisha migongano ya mara kwa mara kati ya nchi husika.
Alisema kutambuliwa kwa mipaka rasmi kutasaidia kuondoa migogoro, hasa pale inapotokea kuvumbuliwa kwa madini na rasilimali nyingine kwenye mipaka ya nchi husika.
Alisema ni robo tu ya mipaka katika nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara, ndiyo isiyokuwa na migogoro. Mwaka jana kwenye Mkutano wa Wakuu wa Umoja wa Afrika (AU) kuliongezwa muda wa kumaliza matatizo ya mipaka hadi mwaka 2017.
Aliipongeza Serikali ya Shirikisho ya Ujerumani kwa kuwezesha kukamilika kwa kazi ya upimaji mipaka kati ya Tanzania, Ushelisheli na Comoro. Serikali hiyo imekuwa mwezeshaji mkuu wa Programu ya Mipaka ya AU (AUBP).
“Baadhi ya mipaka inachorwa kwa bunduki na damu, tumechagua kuchora mpaka wetu kwa kalamu na wino. Tumekitendea haki kizazi chetu kijacho…tuiepushe Afrika na migogoro…,” alisema Membe.
Saturday, February 18, 2012
YANGA NA ZAMALECK UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR LEO
Mshambuliaji wa Timu ya Yanga,Khamis Kiiza akishangilia goli lake la kwanza alilolipachika dakika ya 36 ya mchezo huo dhidi ya Zamaleck ya Misri kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo.
Khamis Kiiza akishangilia na Mashabiki wa Yanga mara baada ya kufunga goli la kwanza.
ubao unavyosomeka.
Beki wa Yanga,Nadir Haroub akichuana vikali na Mshambuliaji wa Zamaleck,Omotoyosi Razack.
Hatati langoni mwa timu ya Zamaleck.
MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AMJULIA HALI MWASISI WA ASP NA TANU, COSTANTINE MILLINGA
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,akizungumza na Mwasisi wa Chama cha ASP na TANU, Costantine Osward Millinga (91) anayesumbuliwa na maradhi, wakati alipomtembelea kumjulia hali nyumbani kwake Kijiji cha Mhekela Wilaya ya Mbinga.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,akizungumza na Mwasisi wa Chama cha ASP na TANU, Costantine Osward Millinga (91) anayesumbuliwa na maradhi,wakati alipomtembelea kumjulia hali nyumbani kwake Kijiji cha Mhekela Wilaya ya Mbinga.Katikati ni Mke wa Makamu Mama asha Bilal na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu.
Mke wa Makamu Mama Asha Bilal akimsalimia mwasisi huyo.Picha na Muhidin Sufiani-OMR.
Rais Kikwete aongoza matembezi ya hisani kusaidia ujenzi wa hospitali ya kinamama ya CCBRT jijini Dar
Rais Kikwete akiongoza matembezi ya Hisani kuchangia ujenzi wa hospitali ya kinamama ya Baobab iliyo chini ya CCBRT jijini Dar es salaam. Katika picha kutoka kulia Meya wa Ilala Mh Jerry Silaa, Meya wa Kinondoni Mh Mwenda, Bw Erwin Telemans Mkurugenzi mtendaji wa CCBRT, Rene Meza Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya CCBRT Bw. Wilbroad Slaa na kulia kwa Rais ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Hadji Mponda na Mkurugenzi wa Vodafone Foundation Bw. Andrew Dunnet pamoja na Mwamvita Makamba wa Vodacom Tanzania katika matembezi hayo leo asubuhi.
Rais Jakaya Kikwete akishiriki katika mazoezi ya viungo kabla ya kuongoza matembezi ya hisani kuchangia ujenzi wa hospitali ya kinamama matatizo mbalimbali ya uzazi katika hospitali ya CCBRT leo asubuhi jijini Dar es salaam. Matembezi hayo yameanzia katika hoteli ya Golden Tulip na kumalizika katika Hospitali ya CCBRT Mikocheni, matembezi hayo yameandaliwa kwa pamoja na kampuni ya Vodacom Tanzania, Vodafone pamoja na hospitali ya CCBRT Kampeni hiyo inaitwa Find your Moyo.
Naombeni Maelezo ya Picha Hii Wadau
Friday, February 17, 2012
Vodacom yaadhimisha siku ya wateja wa kampuni hiyo leo jijini Dar
Wasanii wakiburudisha wakati wa Promosheni kuazimisha siku ya wateja wa kampuni hiyo ambapo wafanyakazi wa kampuniya Vodacom walienda mitaani kuelimisha wateja kuhusu huduma ya m-pesa na promosheni zinazoendelea za punguzo la utumaji fedha la asilimia 75 na bonasi hadi asilimia 25 unaponunua muda wa hewani kupitia m-pesa.
Msafara wa magari ya Vodacom Tanzania ukipita katika barabara ya Morogoro maeneo ya Manzese jijini Dar es Salaam yakiwabeba wafanyakazi wa kampuni hiyo leo wakati wa kuadhimisha siku ya wateja wa kampuni hiyo ambapo wafanyakazi wa kampuni hiyo walienda mitaani kuelimisha wateja kuhusu huduma ya m-pesa na promosheni zinazoendelea za punguzo la utumaji fedha la asilimia 75 na bonasi hadi asilimia 25 unaponunua muda wa hewani kupitia m-pesa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene Meza akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa kuadhimisha siku ya wateja wa kampuni hiyo ambapo wafanyakazi wa kampuni hiyo walienda mitaani kuelimisha wateja kuhusu huduma ya m-pesa na promosheni zinazoendelea za punguzo la utumaji fedha la asilimia 75 na bonasi hadi asilimia 25 unaponunua muda wa hewani kupitia m-pesa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene Meza akizindua msafara wa magari wakati wa kuadhimisha siku ya wateja wa kampuni hiyo ambapo wafanyakazi wa kampuni hiyo walienda mitaani kuelimisha wateja kuhusu huduma ya m-pesa na promosheni zinazoendelea za punguzo la utumaji fedha la asilimia 75 na bonasi hadi asilimia 25 unaponunua muda wa hewani kupitia m-pesa.Kushoto Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa kampuni hiyo Mwamvita Makamba.
Mmoja wa wafanyakazi wa Vodacom Tanzania akibandika tangazo linaonyesha huduma za m-pesa wakati wa kuadhimisha siku ya wateja wa kampuni hiyo ambapo wafanyakazi wa kampuni hiyo walienda mitaani kuelimisha wateja kuhusu huduma ya m-pesa na promosheni zinazoendelea za punguzo la utumaji fedha la asilimia 75 na bonasi hadi asilimia 25 unaponunua muda wa hewani kupitia m-pesa.
Baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania wakiwa katika mitaa ya Mbagala jijini Dare s Salaam wakitembea kwenda kuwaelimisha wateja wao wakati wa kuadhimisha siku ya wateja wa kampuni hiyo ambapo wafanyakazi wa kampuni hiyo walienda mitaani kuelimisha wateja kuhusu huduma ya m-pesa na promosheni zinazoendelea za punguzo la utumaji fedha la asilimia 75 na bonasi hadi asilimia 25 unaponunua muda wa hewani kupitia m-pesa.
Mzee Said Ally mkazi wa Mbagala akipewa maelekezo na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania juu ya huduma ya m-pesa wakati wa Promosheni kuadhimisha siku ya wateja nchini nzima ambapo wafanyakazi wa kampuni hiyo walienda mitaani kuelimisha wateja kuhusu huduma ya m-pesa na promosheni zinazoendelea za punguzo la utumaji fedha la asilimia 75 na bonasi hadi asilimia 25 unaponunua muda wa hewani kupitia m-pesa.
Baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania wakibandika matangazo katika moja ya kibanda cha duka Mbagala Zakiemu yakionyesha huduma za m-pesa wakati wafanyakazi hao walipokuwa wakiadhimisha siku ya wateja ambapo wafanyakazi wa kampuni hiyo walienda mitaani kuelimisha wateja kuhusu huduma ya m-pesa na promosheni zinazoendelea za punguzo la utumaji fedha la asilimia 75 na bonasi hadi asilimia 25 unaponunua muda wa hewani kupitia m-pesa.
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Vodacom imeanza kuwatembelea wateja wao nchi nzima ili kujua changamoto gani ambazo wanakutana nazo baada ya kuzindua promosheni ya punguzo la huduma ya kutuma pesa (M-pesa) kwa asilimia 75.
Pamoja ya kujua changamoto za huduma hiyo pia kampuni hiyo imeangalia jinsi wateja wake walivyo pokea huduma hiyo muhimu.
Akizungumza mjini Dar es Salaam jana Mkurugenzi mtendaji wa Vodacom Rene Meza alisema kwa kutambua umuhimu wa wateja wao hapa nchini kampuni hiyo imetenga siku muhimu ijulikanayo kama ‘Siku ya masoko’ ili kuangalia jinsi gani wateja wao walivyo elewa na kuzipokea huduma zao.
“Wafanya kazi wote wa Vodacom nchi nzima leo (jana) wakiongozwa na wakurugenzi na washiriki wote wa kampuni yetu wata watembelea mawakala na wananchi ili tuangalia changamoto gani wanazokutana nazo na kusikiliza ushauri wao.
“ Tatizo la mawasilianio ni kubwa sana tumekuwa tukipata malalamiko kutoka kwa wateja wetu hivyo kwa kutumia siku hii muhimu tutajua matatizo yote ambayo wateja wetu wanakutana nayo,”alisema Meza.
Naye Afisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Mwamvita Makamba alisema huduma ya M-pesa imerahisisha maisha kwa wananchi wa hali zote hapa nchini kwani kwa kutumia huduma hiyo wateja wameweza kulipia huduma ya Luku pamoja na ada kwa wanafunzi bila matatizo.
Kampuni ya Vodacom imeweka kianzio cha Sh 50 cha kutuma pesa na bonas ya asilimia 25 kwa wateja wake ambayo itaenda sambamba na zawadi ya kitita cha Sh milion 480 kushindaniwa.
Maeneo ambayo yametembelea na Vodacom kwa Dar es Salaam ni pamoja na Kariakoo, Tegeta, Kimara,mbezi pamoja na Mbagala.





































